Vigezo vya Matumizi yaFamilySearch
imesasishwa 9/1/2023
Kuna utofauti kulingana na mazingira husika pale inapohitajika kisheria
Kwa kutumia tovuti hii, unakubaliana na masharti yaliyowekwa hapo chini ya (“Makubaliano” haya). Kama hukubaliani na kifungu chochote cha masharti ya Makubaliano haya, basi usitumie tovuti hii. Tunayo haki ya kubadilisha Makubaliano haya wakati wowote, hivyo tafadhali kagua mabadiliko kwenye Makubaliano haya kila wakati unapotumia tovuti hii. Kuendelea kwako kutumia tovuti hii kufuatia kuwekwa kwa mabadiliko kwenye Makubaliano haya humaanisha kwamba unayakubali mabadiliko hayo.
Leseni na Vizuizi
Tovuti hii ni maalum kwa ajili ya historia ya familia na utafiti wa nasaba, inasimamiwa na FamilySearch International, shirika lisilo la kibiashara la Utah lenye ofisi zake kuu huko Salt Lake City, Utah, Marekani (“FamilySearch”, “sisi”, “-yetu””, au neno la jinsi hiyo) shirika lisilo la kibiashara ambalo linahusiana na “Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho (“Kanisa”) Taarifa zote zinazopatikana kwenye tovuti hii (ikijumuisha picha, maandishi, ikoni, maonyesho, kanzidata, vyombo vya habari, bidhaa, huduma, na habari) zinamilikiwa au zimepewa leseni na sisi.
Isipokuwa imeonyeshwa vinginevyo, unaweza kutazama, kupakua, na kuchapisha taarifa kutoka kwenye tovuti hii kwa matumizi yako binafsi tu, matumizi yasiyo ya kibiashara, au kwa matumizi yako kama mtu anayejitolea kwenye uwekaji taarifa anayehusiana na Programu ya FamilySearch Indexing kwa mujibu wa Vigezo na Masharti ya Programu ya FamilySearch Indexing au FamilySearch Indexing Software Licence Agreement.
Hauruhusiwi kutuma maudhui kutoka kwenye tovuti hii kwenda tovuti nyingine au kwenye mtandao wa kompyuta pasipo ruhusa yetu. Hauruhusiwi kusambaza au kugawa maudhui kutoka kwenye tovuti hii kwenda tovuti nyingine. Hauruhusiwi kutumia tovuti hii au habari zinazopatikana kwenye tovuti hii (ikijumuisha majina na anwani za wale ambao wametuma taarifa zao) ili kuuza au kuzitangaza bidhaa au huduma, ili kutafuta wateja, au kwa kusudi lolote la kibiashara.
Wataalamu wa nasaba wanaweza kutumia tovuti hii, au programu za simu ya mkononi, au nyenzo za kituo cha FamilySearch ili kutafiti taarifa kwa ajili ya na kutoa nyaraka kwa ajili ya matumizi ya mtumiaji yasiyo ya kibiashara. Hata hivyo, wataalamu wa nasaba hawapaswi kutafuta au kupanga biashara, kujitangaza, au kupokea malipo kupitia tovuti hii au kupitia vitu ambavyo tunavimiliki.
Kama nyongeza, taarifa kutoka kwenye tovuti hii zinaweza kuzalishwa na wafanya kazi wa vyombo vya habari kwa matumizi katika majukwaa ya habari za umma isipokuwa imeonyeshwa vinginevyo. Matumizi mengine ya habari au nyenzo zinazopatikana kwenye tovuti hii, ikijumuisha kila matumizi ya shirika au taasisi kisheria, hayaruhusiwi bila ruhusa ya maandishi kutoka kwetu. (Ona “Ruhusa ya Kutumia Hakimiliki na Alama ya Biashara” hapo chini.)
Licha ya hayo yaliyotangulia, tunayo haki kulingana na busara yetu wenyewe ya kukataa, kubatilisha, au kuweka kikomo cha matumizi ya tovuti hii, ikijumuisha uzalishaji upya na matumizi mengine yoyote ya nyenzo zipatikanazo kupitia tovuti hii. Siyo wajibu wetu, hata hivyo, kuamua, “matumizi halali” humaanisha nini kwa mtu anayetamani kutumia nyenzo kutoka tovuti hii. Hiyo hubakia kuwa wajibu wa mtumiaji wa tovuti hii. Zaidi ya hayo, hatuhitajiki kutoa vyanzo vya ziada vya marejeleo, au kutoa hakikisho kwamba nyenzo zilizo kwenye tovuti hii zinaweza kutumika kwenye matumizi mengine yoyote mbadala. Wajibu kama huu pia unabakia kwa mtumiaji binafsi wa tovuti hii. Hata hivyo, tunayo haki ya kuzuia ukiukwaji wa matumizi ya nyenzo zetu na kutoa tafsiri ya “matumizi sahihi” kwa kadiri tunavyoelewa kisheria.
Tovuti hii haikusudiwi kutumika katika Shirikisho la Urusi na hivyo, haipaswi kutumiwa ndani ya Shirikisho la Urusi.
Ruhusa ya Kutumia Hakimiliki na Alama za Biashara
Ili kuomba ruhusa ya matumizi ya nyenzo zetu au za wale tunaohusiana nao zenye haki miliki au alama za biashara, tafadhali fuata kiunganishi hiki:
Zingatia: Makadirio ya muda wa kupokea majibu ya ombi lako ni siku 45. Maombi yanayohusisha idadi kubwa ya taarifa yanaweza kuchukua muda mrefu zaidi.
Maombi mengine
Aina nyingine za maombi inaweza kutumwa kwenye moja ya tovuti hizi.
-
FamilySearch: Maswali au maombi yanayohusiana na FamilySearch yanaweza kushughulikiwa kupitia FamilySearch Support au FamilySearch Help and Learning.
-
Maktaba ya Historia ya Kanisa: Maswali yanayohusiana na nyenzo zinazopatikana kwenye Maktaba ya Historia ya Kanisa yanapaswa kutumwa kupitia Church History Library Catalog.
-
Usimamizi wa Akaunti: Maswali yanayohusiana na usimamizi wa akaunti yanaweza kujibiwa kwenye Account Help.
Masharti ya Usajili
Kwa kuamua kutumia tovuti hii, unaonesha kwamba (a) umesoma na kukubali vigezo vya Makubaliano haya, na (b) kisheria umeweza kujisajili (kama inahitajika) ili kutumia tovuti hii na tovuti nyingine yoyote inayohusiana na FamilySearch. Kama utawasilisha taarifa yoyote binafsi kwenye tovuti hii, unakubali kutoa taarifa iliyo ya kweli, sahihi, na ya sasa kuhusu wewe mwenyewe (ikijumuisha wakati wa mchakato wa kujisajili) na kudumisha na kufanya kuwa ya sasa na sahihi taarifa hii kukuhusu kama itakuwa na mabadiliko. Kama utatoa taarifa ya uongo, isiyo sahihi, isivyostahili, au maandishi ya taarifa au picha ya kukashifu, tunaweza kuisimamisha au kuitoa au kuifuta akaunti yako na utumiaji wako wa tovuti hii. Wakati wa mchakato wa usajili, utaombwa kubuni jina na neno siri ili kuzifikia sehemu fulani za hii tovuti au tovuti nyinginezo zinazohusiana na FamilySearch. Unawajibika katika utunzaji wa usiri wa jina lako la kuingilia katika akaunti yako pamoja na nywila yako. Unawajibika kwa shughuli zote ambazo zinatokea kwa kutumia jina lako la kuingilia na nywila. Kama mtu mwingine anatumia jina lako la kuingilia na nywila yako katika njia ambayo inavunja masharti ya Makubaliano haya, unawajibika kwa vitendo vya mtu huyo, na matumizi ya jina lako la kuingilia yanaweza kusimamishwa au kuondolewa.
Leseni na Haki Tulizopewa
Kama mabadilishano kutokana na matumizi yako ya tovuti hii na/au uhifadhi wetu wa aina yoyote ya data unayowasilisha, unatupatia leseni isiyo na kikwazo, isiyohitaji malipo, isiyohitaji mrabaha, ya ulimwenguni kote, inayoweza kutolewa kwa wengine, na endelevu ya kutumia taarifa zote, maudhui, na nyenzo zingine (kwa ujumla, “Maudhui Yaliyowasilishwa”) ambazo umeziwasilisha au vinginevyo unazitoa kwenye tovuti hii (ikijumuisha, bila kikomo, data za nasaba, taswira, picha, maandishi, nyaraka, taarifa, rekodi, majadiliano, habari, na data zinazohusiana na mtu aliyefariki au kitu kingine chochote) kwa ajili ya madhumini yoyote au yote, katika namna yoyote na zote, na kwa namna yoyote na aina zote za vyombo vya habari, ambavyo sisi, kwa uamuzi wetu pekee, tunaona inafaa kwa ajili ya kuendeleza dhamira yetu ya kukuza historia ya familia na utafiti wa nasaba. Kama sehemu ya leseni hii, unatupatia ruhusa ya kunakili, kuonyesha kwa umma, kusambaza, kutangaza, kutenda hadharani, kugawa, na vinginevyo kutumia (na kuwaruhusu wengine kutumia) Maudhui Yaliyowasilishwa) kote ulimwenguni, kwa njia yoyote tuonayoona inafaa (kielekroniki au vinginevyo, ikijumuisha kwenye mtandao). Pia unaelewa na kukubali kwamba kama sehemu ya leseni hii, tunayo haki ya kutengeneza (na kuruhusu wengine kutengeneza) na kutumia kazi zinazotokana na Maudhui yako Yaliyowasilishwa kwa kuunganisha yote au sehemu yake na yale ya wachangiaji wengine au vinginevyo kwa kurekebisha Maudhui yako Yaliyowasilishwa.
Ushirikiano na Wengine
Unakubali kwamba dhumuni la msingi la tovuti hii ni kuwezesha ushirikiano baina ya watumiaji wa tovuti hii na tovuti nyinginezo ambao wanataka kupanua kanzidata zao na maarifa yao ya nasaba. Unakubali kwamba tunaweza kutumia Maudhui Yaliyowasilishwa, ikijumuisha taarifa yoyote binafsi ya watu walio hai, ambayo unaiwasilisha kwa dhumuni la kushirikiana na kushiriki na watu wengine binafsi na mashirika (ikijumuisha mashirika ya kibiashara ya nasaba) ili, kwa mfano, kuunda hesabu ya vizazi ya ulimwenguni kote kwa madhumini ya kuongeza ushiriki katika historia za familia na kuhifadhi kumbukumbu ulimwenguni kote. Unakubali kwamba ushirikiano baina ya watu wengine binafsi na mashirika unaturuhusu kupata data za nyongeza ambazo tunaweza kuwapatia watumiaji kwenye tovuti hii—hivyo kuruhusu watumiaji kuongeza idadi ya familia za vizazi vyao.Taarifa yetu ya Faragha inatoa maelezo ya kina zaidi kuhusu utumiaji wetu wa Maudhui Yaliyowasilishwa.
Unakubali kuingiza data kwa usahihi kwa maarifa yako yote. Ili kudumisha uthabiti katika mwonekano asili wa nasaba unaopatikana kwenye tovuti hii (kama vile chati za ukoo, chati ya mwonekano wa mlalo, chati za mduara, na mwonekano na chati zingine), unakubali kuwatambua watu kwa jinsia yao ya kibaiolojia na kuwaingiza katika nafasi zao kwa asili za mwanamume au mwanamke kwenye chati na mwonekano (mfano, baba au mama). Katika ndoa za jinsia moja, wanandoa wote watakuwa wa jinsia moja. Unaweza kuingiza muhtasari wowote unaohusu utambulisho wa jinsia katika maoni. Tafadhali rejelea sehemu ya Kanuni ya Maadili kwa ajili ya muhtasari wa matokeo yamkini kwa kuingiza data isivyo sahihi.
Tovuti hii inajumuisha makala ya majadiliano ambapo watu binafsi wanaweza kutoa maoni na vinginevyo kutoa Maudhui Yaliyowasilishwa kuhusiana na mtu aliyefariki na kutoa maelezo kuhusiana na mfu huyo. Tunayo haki ya kutumia tena taarifa za majadiliano hayo na Maudhui mengine Yaliyowasilishwa yaliyotolewa na kuyachapisha kwa wengine katika jitihada za kusaidia kutatua changamoto za wazi zilizoonekana au kusaidia kuwaelimisha wengine. Tunakuomba uwe makini katika kuchagua taarifa unazozijumuisha katika majadiliano yako mtandaoni na Maudhui mengine Yanayowasilishwa, badala yake wasiliana kupitia barua pepe au kwa njia nyingine wakati ambapo taarifa binafsi za mawasiliano au mambo mengine binafsi, au taarifa nyeti inapokuwa inatolewa. Unakubali kwamba vitu vyovyote unavyowasilisha kupitia kipengele cha majadiliano vitaweza kuonwa na mtu yeyote anayeweza kuifikia tovuti hii. Kipengele cha majadiliano kinakusudiwa kusaidia juhudi za ushirikiano, kuratibu, masahihisho ya makosa, na kuwezesha utafiti wa ziada pamoja na watumiaji wengine wanaopenda. Kipengele cha majadiliano kinaweza (a) kisitumiwe kwa sababu isiyohusiana na mada inayojadiliwa, (b) kisijumuishe taarifa ambayo inaweza kumdhuru au kumwaibisha mtu yeyote aliye hai, au (c) kisijumuishe lugha au maudhui yenye kumchokoza mtu, yasiyo ya heshima, yasiyo sahihi, ya kutishia, au ya matusi. Kutokukubaliana kuhusu ukweli unaomhusu mtu aliyefariki inawezekana sana kutokea, na kutokukubaliana kwa aina hiyo kunapaswa kuwekwa wazi katika masharti ya wazi kulingana na kweli na vyanzo tajwa inapowezekana, pasipo kukimbilia lugha ya jazba, matusi, au lugha au maoni yasiyo ya ukarimu. Kipengele cha majadiliano kinaweza kisitumike kutoa viunganishi kwenda tovuti za nje pamoja na maudhui yasiyo sahihi (ingawa viunganishi vya taarifa husika na zenye taarifa kuhusiana na mfu vinaweza kuwa sahihi) au ili kutafuta biashara au kutoa huduma za utafiti. Ingawa hatulazimiki kufanya hivyo, tunayo haki, kulingana na busara yetu wenyewe, kufuta au kuhariri Maudhui Yaliyowasilishwa yaliyotolewa katika kipengele cha majadiliano na vipengele vingine sawa na hicho na kuzuia ufikiaji wa mtu wa vipengele hivyo kwa sababu yoyote au bila sababu. Tafadhali rejelea sehemu ya Kanuni ya Maadili kwa ajili ya muhtasari wa matokeo yamkini kwa ajili ya matumizi yasiyo sahihi ya kipengele cha majadiliano na vipengele sawa na hicho.
Programu ya Kompyuta
Kama unaweza kupakua programu kutoka tovuti hii, unaweza kuitumia programu hiyo kama ilivyotolewa na makubaliano ya leseni ambayo inaambatana na programu hiyo. Ni wewe pekee unayewajibika kwenye kutii masharti yoyote ya usafirishaji ya Marekani ambayo yanaweza kutumika kwenye programu yoyote inayotolewa kwenye tovuti hii.
Haki ya Kuwasilisha
Maudhui yoyote unayoyawasilisha kwenye tovuti hii yako chini ya Makubaliano haya na kwenye FamilySearch Content Submission Agreement. Unawakilisha na kuhakikisha kwamba hutawasilisha kitu chochote kwenye tovuti hii ambacho kinakiuka haki yoyote ya mtu mwingine (ikijumuisha, lakini siyo kwa ukomo, haki miliki, haki za faragha, haki za utangazaji, haki za kimikataba, au haki zingine za umiliki). Wakati wowote unapowasilisha Maudhui Yaliyowasilishwa kwenye tovuti hii unathibitisha kwamba unayo haki kisheria ya kuwasilisha Maudhui hayo kwetu na unatupatia sisi pamoja na washirika wetu haki na leseni zilizowekwa kwenye Makubaliano haya na katika Makubaliano ya FamilySearch Content Submission. Unakubali kuwajibika kisheria kwa matumizi yoyote ya Maudhui Yaliyowekwa ambayo unayawasilisha. Ni wewe pekee unayewajibika kwa Maudhui Yaliyotolewa unayoyawasilisha, kuchapisha, au vinginevyo kuyaleta kwenye tovuti hii au kwenye tovuti nyingine yoyote inayoshirikiana na FamilySearch.
Kuwasilisha Majina kwa ajili ya Ibada za Kidini
Unapaswa kuwasilisha majina pekee ya watu wa ukoo wa familia yako mwenyewe kwa ajili ya ibada za kidini kwa uwakilishi, na hupaswi kuwasilisha majina ya watu usio na undugu nao kama vile wasanii maarufu au watu mashuhuri, au majina yaliyokusanywa kutoka miradi ya utafiti, isiyoidhinishwa, kama vile, wahanga waMauaji ya Kimbari ya Wayahudi.
Kanuni ya Maadili
Unakubali kwamba hutafanya kama mtu binafsi, au kama sehemu ya juhudi yoyote ya pamoja, kuwasilisha au kuweka taarifa kwenye tovuti hii (ama wakati wa usajili kama wasilisho la nasaba kupitia makala za majadiliano au kupitia makala nyingine yoyote ambapo Maudhui Yaliyowasilishwa yanaweza kutolewa) ambayo yanaweza kuonekana kuwa na madhara au kukera wengine. Pia unakubali kutoiga mtumiaji mwingine kwa dhumuni lolote, ikijumuisha kuficha utambulisho wako, au kumhusisha mtu mwingine kwa matendo yako. Pia unakubali kutotafuta, kukusanya au kutumia taarifa yoyote kutoka tovuti hii katika namna ambayo inaweza kudhuru, kutofautisha, kunyanyasa, au kuathiri mtu au chombo chochote. Zaidi unakubali kwamba isipokuwa kama umepokea kibali chetu kwa maandishi hutatumia programu yetu ya kompyuta, teknolojia, au kifaa kupakua kwa wingi, kufuta maudhui, au kwa maana nyingine kuchukua taarifa yoyote au habari kutoka kwenye tovuti hii. Unakubali kutokwepa udhibiti wowote au sheria za utumiaji ambazo tumetekeleza. Unakubali kutozalisha tena, kurudufu, kutoa nakala, kupakua, kusambaza, kuonyesha, kufanya ipatikane kwa umma, kuuza, au vinginevyo kutumia sehemu yoyote ya tovuti hii au taarifa zake kwa matumizi yoyote yasiyo ya binafsi au matumizi ya kibiashara. Unakubali kutojihusisha na shughuli yoyote inayohusiana na tovuti hii, maudhui yake, au watumiaji wake ambayo inaweza kujumuisha kosa la jinai au kile ambacho kinaweza kuibua uwajibikaji wa kisheria. Zaidi ya hayo, unakubali kutochapisha upya, kutangaza kwa umma, kusambaza, kugawa, kutenganisha, kuiga, kubadilisha mhandisi, kuunda kazi zinazotokana na, au kuunda upya tovuti, huduma zake, msingi wa tovuti, au maudhui pasipo kwanza kupata ruhusu yetu ya maandishi. Zaidi unakubali kutofanya lolote ambalo linaweza kutatiza mtiririko wa data kwenda au kutoka kwenye tovuti hii au kuathiri huduma au utendaji wa tovuti hii. Unaelewa kwamba matokeo ya vitendo vyenye madhara au vyenye kukera au ukiukaji mwingine wowote wa Makubaliano haya, unaweza kujumuisha ubatilishaji wa haki yako ya kutumia tovuti hii, (ikijumuisha tovuti nyingine yoyote ya FamilySearch au aplikesheni za simu ya mkononi, na nyenzo nyingine yoyote kutoka huko) na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Utunzaji wa Mawasilisho
Tunakusudia kutumia juhudi zinazofaa kuhifadhi uadilifu wa Maudhui yako Yaliyowasilishwa na kuepuka makosa au kuondolewa kwa maudhui ya tovuti hii. Hata hivyo, unakubali kwamba hatutawajibishwa wala kuwajibika kwa makosa au kuondolewa kwa maudhui yoyote unayoweza kuyaona kwenye tovuti hii, wala kwa upotevu, au uharibifu, au upotovu wa Maudhui Yaliyowasilishwa ambayo unayawasilisha au unayatuma.
Kuunganisha
Kwa ajili ya msaada kwako, tovuti hii inaweza kuwa na viunganishi vingi kwenda tovuti nyingine zinazoendeshwa na watu wengine. Hivyo tovuti za watu wengine hazisimamiwi au kudhibitiwa na sisi, nahatuwajibikikwa maudhui yao. Ingawa tunaamini tumefanya jitihada za nia njema kuhusisha tovuti nzuri, zinazofaa, baadhi zinaweza kuwa na taarifa zisizo sahihi au zenye pingamizi. Ikiwa utapata taarifa za jinsi hii wakati ukitumia tovuti ambayoumeifikiakupitia kiunganishi kwenye tovuti hii, tafadhalitujulishemara moja.
Tunaamini kwamba wale wanaofanya taarifaipatikanekwenyeintanetiwanatarajia kwamba itakuwa inapatikana kwa umma na ulimwenguni kote. Kwa hiyo, tunaamini kwamba kuunganisha kwenye tovuti nyingine kisheria inaruhusiwa na ni sambamba na matarajio ya wale wanaotumiaintaneti. Hata hivyo, kama ufikiaji kwenye tovuti maalum unapaswa kuzuiliwa, mwendeshaji wa tovuti kama hiyo anapaswa kutujulisha haraka sana.
Faragha na Ulinzi wa Data
Kwa kutumia tovuti hii na kuwasilisha data zako binafsi kwetu, unatoa idhini yakuchakatanchini Marekani au maeneo mengine data yoyote binafsi ambayounaiwasilishakwa mujibu wa Notisi yetu ya Faragha. Pia unakubali kutii sheria zote zinazotumika kuhusu usambazaji wa data binafsi kwenda au kutoka Marekani na katika nchi unayoishi.
Mamlaka ya Kisheria na Sheria Inayotumika
Makubaliano haya yatatawaliwa na sheria za Jimbo la Utah, Marekani, kama inavyotumika kwenye makubaliano yaliyoingiwa na kufanyika tu ndani ya jimbo hili, pasipo kutoa nafasi kwa chombo chochote cha migogoro ya kisheria. Tendo lolote unaloleta ili kuimarisha Makubaliano haya au mambo yoyote yanayohusiana na tovuti hii yataletwa katika ama mahakama ya jimbo au mahakama za shirikisho zilizoko jimbo la Salt Lake, Utah, na hapa unakubali na kuridhia maamuzi binafsi ya mahakama hizo kwa madhumuni ya kutoa maamuzi juu ya tendo uliloleta. Unakubali hili bila kujali eneo uliko au usumbufu wowoteutakaoupata. Kama kuna masharti yoyote ya Makubaliano haya ambayo ni kinyume cha sheria, yasiyo na nguvu ya kisheria, yasiyotekelezeka kwa ujumla au kwa sehemu, masharti yanayobaki hayatatumika, isipokuwa tukibaini kuwa sharti hilo ni batili au halitekelezeki, ni sehemu muhimu katika Makubaliano haya, katika hali hiyo tunaweza kwa busara yetu wenyewe kurekebisha Makubaliano haya.
Ukomo wa Uwajibikaji
Hatuwajibiki kwa uharibifu wowote maalum au uharibifu wa matokeo yanayotokana na matumizi yako au kutokuwa na uwezo wa kutumia tovuti hii au taarifa katika tovuti hii au tovuti yoyote iliyounganishwa, ikijumuisha, lakini bila ukomo kwenye, faida iliyopotea, kukatizwa kwa biashara, upotevu wa programu, au data, kwenye mfumo wako wa kushughulikia taarifa. Katika lolote, hatuwajibiki kwako kwa sababu ya uharibifu, hasara, na tendo lolote unalolifanya, kwa kutumia tovuti hii au yoyote iliyounganishwa na hii.
Kanusho
TOVUTI HII NA NYENZO KATIKA TOVUTI HII NA TOVUTI YOYOTE ILIYOUNGANISHWA NAYO VIMETOLEWA “KAMA VILIVYO” NA BILA DHAMANA YA AINA YOYOTE ILE YA MAANDISHI AU UTENDAJI. KWA KIWANGO KAMILI KINACHORUHUSIWA KWA MUJIBU WA SHERIA INAYOTUMIKA, TUNAKANUSHA DHAMANA ZOTE ZA MAANDISHI, AU UTENDAJI, IKIWEMO LAKINI BILA KIKOMO, DHAMANA YA HATI, NA DHAMANA INAYOHUSISHWA YA UDHIBITI WA UUZAJI NA USIMAMIZI KWA DHUMUNI HUSIKA. HATUTOI HAKIKISHO KWAMBA KAZI ZA TOVUTI HII HAZITAINGILIWA AU ZITAKUWA HAZINA MAKOSA, BALI KWAMBA KASORO HIZO ZITASAHIHISHWA, AU KWAMBA TOVUTI HII AU MTOA HUDUMA ANAYEIFANYA IPATIKANE NI SAFI DHIDI YA VIRUSI VYA KOMPYUTA AU VITU VINGINE HATARISHI.
Alama za biashara
Ifuatayo ni orodha ya baadhi ya alama zetu za biashara na za huduma na za washirika wetu:
- FamilySearch
- FamilySearch GEDCOM
- International Genealogica lIndex
- RootsTech
- The Church of Jesus Christ of Latter-day Saints
Alama hizi ni vitambulishaji vya FamilySearch au Intellectual Reserve, Inc. Na zimesajiliwa huko Marekani na nchi zingine. Kwa taarifa za ziada kuhusu alama zetu za biashara na huduma na za washirika wetu na matumizi yake sahihi, tafadhali ona Miongozo ya kutumia alama ya biashara za FamilySearch.
Maswali
Kwa usaidizi zaidi au taarifa kuhusu alama za biashara na nyenzo zetu za hakimiliki na za washirika wetu, unaweza kuwasiliana na ofisi yetu yaIntellectualPropertykwa:
simu: 1-801-240-3959or1-800-453-3860,ext. 2-3959
Faksi: 1-801-240-1187
Barua pepe: cor-intellectualproperty@FamilySearch.org
Imesasishwa: 9/1/2023